Ona aibu Mwanaume kutunzwa na nyumba ndogo

Najua nikisema sana nitaonekana kuwa nina mdomo wakati kila kiumbe hapa duniani kina mdomo, lakini kwa vile kuwapasha ndiyo ‘hobi’ yangu acha niwachane ‘live’ simuogopi mtu hasa wewe mwenye hila ya kwapa kunuka bila kidonda.

Mambo mengine unaweza kuona kama ni kichekesho, kwa vile mimi nyani mzee niliyeishi muda mrefu na kukutana na shuruba za porini, siwezi kuliacha hivi hivi likapita kwani aibu hii inashusha heshima ya ndoa.
Siku hizi nyumba ndogo siyo siri tena, sasa hivi asilimia tisini ya wanandoa lazima wanakuwa na vidumu. Nakuona mnatazamana na mkeo, ukweli ni huo wewe unayedai wako kwa ajili ya kukushikia gari ikiwa umechoka uongo?
                                                  
Wenye ndoa tumekuwa ndiyo hasa tukiwalazimisha waume zetu wazitafute raha nje baada ya ndani kukosekana. Nilielezea wiki jana jinsi wanawake tunaposhindwa kujitambua tukiachika tunasema tumerogwa kumbe wachawi ni sisi wenyewe.
Juzi kuna mwanamke shoga yangu wa karibu alinieleza kitu kilichonihuzunisha sana. Shoga yangu mwenyewe mwingi wa habari anawapenda waume za watu ambao anasema wanajua kutunza si waongo kama masingo. Kama kawaida alimtia mikononi mume wa mtu aliyejipendekeza. Baada ya kukutana naye alichokutana nacho kilimfanya amshushe thamani mkewe na kumuona ni mwanamke kimaumbile lakini hana hulka ya kike.
Anasema baada ya yule mwanaume kukaa mkao wa kula alichokutana nacho kinatia kichefuchefu. Mwanaume chini kichaka kimeota unaweza kusuka tatu kichwa, si huko hata makwapani nako ndiko usiseme mpaka zimebadilika rangi nakuwa za njano. Ikabidi kabla ya mchezo aingie kazini kumsafisha.
Najiuliza hayo mapenzi na mkewe wanafanya gizani na hata kama ni gizani, kwa kutumia mkono hawezi kujua eneo hilo haliko sawa?Kibaya hata aliporudi nyumbani mkewe hakuona mabadiliko yoyote. Kweli huyo mwanamke kapitia mafunzo ya wanawake kumjua mwanaume anatakiwa afanyiwe nini?
Siku nilipooneshwa huyo mwanamke mwenye mume anavyojipenda utashangaa. Yupo smati kila kona ya mwili amechafuka kwa midhahabu lakini kumtunza mumewe sifuri. Nyumba ndogo imekuwa kubwa kutokana na kila kitu kinachomhusu mwanaume anakifanya wewe upo tu unabakia na sifa ya kuolewa lakini unabakia mke jina.
Kwa mtindo huu wanawake wachache watabakia katika ndoa zao. Jamani hata kwa hili mtasema nachonga sana, tuliache hivihivi lipite ili umpe nafasi nyumba ndogo.
Hivi kweli wewe mwanamke unamwachia mumeo na mikucha na minywele kibao hutaki kumnyoa mpaka aende nyumba ndogo? Aaah! Sipendi miye aibu hii imkute mwanamke mwenzangu, hebu mtunze mumeo apendeze, huyo anayetaka kukuibia akose kazi ya kufanya.
Hebu basi tunapowafanyia usafi waume zetu tusiishie kufua tu, bali ni kumfanyia kila kitu kuanzia kucha hadi kumnyoa kila kona ya mwili wake.Nina imani nimesomeka, ila kama unataka kutishia mashuzi wakati unaendesha ukichafua hali ya hewa mimi simo utarudi kijiweni tupige stori.
Ni mimi Anti Nasra Shangingi Mstaafu.
Newer Posts Older Posts

© Copyright Chiriku Mzee

Designed By Chiriku Mzee

Blogger Templates

Back To Top